TAMKO LA BAVICHA KUHUSIANA NA KAULI ILIYOTOLEWA NA MHE.JOHN SHIBUDA
MBUNGE WA MASWA MASHARIKI.
BAVICHA imepokea kwa mshituko mkubwa kauli ya ndugu Shibuda kuwa yeye
atagombea Urais na Meneja wake wa Kampeni atakuwa Mwenyekiti wa CCM ndugu
Jakaya Kikwete, na alitoa kauli hiyo kwenye kikao cha NEC ya CCM.
MAMBO YAFUATAYO YEMETUSHTUA;
1. Katoa Kauli hiyo kwenye kikao cha NEC ya CCM
2. Meneja wa kampeni zake amemtangaza kuwa ni Mwenyekiti wa CCM taifa
Jakaya Kikwete
3. Amesema kuwa hakuna chama kingine chenye uwezo wa kuiongoza nchi kwa
sasa
4. Alitoa tamko hilo kwa niaba ya APRM .
Mambo hayo manne ndio yametushtua na kutufedhehesha sana sisi vijana wa
CHADEMA na ndio maana tumelazimika kutoa kauli kuhusiana na suala hili , na kauli
yetu ni kama ifuatavyo;
1. Kamwe BAVICHA hatutaruhusu mgombea Urais wa CHADEMA meneja wake
wa kampeni awe ni Mwenyekiti wa CCM hata siku moja kwani tunao watu wa
kutosha na wenye uwezo wa kutosha kuifanya kazi hiyo na hatuhitaji msaada
huo .
2. Kamwe hatutaruhusu mgombea urais wa CHADEMA awe anatangaza nia kwenye
vikiao vya CCM kwani hawana mamlaka ya kumteua mgombea wa CHADEMA
na kama Shibuda alikuwa halijui hilo anapaswa kulifahamu kuanzia sasa kuwa
vijana wa CHADEMA hatuchaguliwi mgombea na NEC ya CCM kwani CHADEMA
kuna vikao na taratibu zetu za kuteua wagombea.
3. Kusema kuwa hakuna chama kingine chenye uwezo wa kuongoza nchi ni
kutudhalilisha sisi vijana wa CHADEMA na watanzania wote ambao leo wanaiona
CHADEMA kama tumaini pekee la kuwakomboa, kauli hii tunaamini kama vijana
wa CHADEMA kuwa mamlaka za nidhamu hazitakaa kimya na kuiachia kauli ya
namna hii iachwe bila kutakiwa maelezo ya kina , tutaitisha kikao cha BARAZA
na tutaijadili kauli hii na kuwasilisha mapendekezo yetu kwenye vikao halali
vya chama .
4. Tunapenda kumwambia kuwa kama anaona kuwa yeye haendani na utamaduni
wa chama chetu na anakiona kuwa hakina uwezo wa kuongoza dola anafanya
nini kwenye chama ambacho anona kuwa hakiwezi kuongoza dola? Kwanini
atafute urais kwenye chama ambacho anaona hakiwezi kuongoza dola ?
anawatania watanzania? Ni heri akaenda kwenye hicho ambacho anaamini kuwa
kinaweza kuongoza dola , kwani lengo la chama chochote kile ni kuchukua dola
na sio vinginevyo.
5. Mwisho tunapenda kuwahakikishia vijana wote wa Tanzania na wananchi kwa
ujumla kuwa tayari CHADEMA kimejiandaa kikamilifu kuongoza dola na wasiwe
na hofu na maneno yaliyotamkwa na Mbunge huyu .
6. Natoa wito kwa Vijana wenzangu wote wa CHADEMA kuwa sasa tujiandae
kikamilifu katika kukabiliana na mtu yeyote yule ambaye ataonekana kuwa
kikwazo kwa chama chetu na wananchi kwa ujumla wake katika kuelekea
kuchukua dola 2015 .
Nawatakia kila la kheri katika ujenzi wa chama na tuendeleze operesheni ya ‘Vua
Gamba, Vaa Gwanda’ popote pale tulipo nchini.
Imetolewa leo Dar es Salaam, Mei 16, 2012 na;
John Heche
Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa.
MBUNGE WA MASWA MASHARIKI.
BAVICHA imepokea kwa mshituko mkubwa kauli ya ndugu Shibuda kuwa yeye
atagombea Urais na Meneja wake wa Kampeni atakuwa Mwenyekiti wa CCM ndugu
Jakaya Kikwete, na alitoa kauli hiyo kwenye kikao cha NEC ya CCM.
MAMBO YAFUATAYO YEMETUSHTUA;
1. Katoa Kauli hiyo kwenye kikao cha NEC ya CCM
2. Meneja wa kampeni zake amemtangaza kuwa ni Mwenyekiti wa CCM taifa
Jakaya Kikwete
3. Amesema kuwa hakuna chama kingine chenye uwezo wa kuiongoza nchi kwa
sasa
4. Alitoa tamko hilo kwa niaba ya APRM .
Mambo hayo manne ndio yametushtua na kutufedhehesha sana sisi vijana wa
CHADEMA na ndio maana tumelazimika kutoa kauli kuhusiana na suala hili , na kauli
yetu ni kama ifuatavyo;
1. Kamwe BAVICHA hatutaruhusu mgombea Urais wa CHADEMA meneja wake
wa kampeni awe ni Mwenyekiti wa CCM hata siku moja kwani tunao watu wa
kutosha na wenye uwezo wa kutosha kuifanya kazi hiyo na hatuhitaji msaada
huo .
2. Kamwe hatutaruhusu mgombea urais wa CHADEMA awe anatangaza nia kwenye
vikiao vya CCM kwani hawana mamlaka ya kumteua mgombea wa CHADEMA
na kama Shibuda alikuwa halijui hilo anapaswa kulifahamu kuanzia sasa kuwa
vijana wa CHADEMA hatuchaguliwi mgombea na NEC ya CCM kwani CHADEMA
kuna vikao na taratibu zetu za kuteua wagombea.
3. Kusema kuwa hakuna chama kingine chenye uwezo wa kuongoza nchi ni
kutudhalilisha sisi vijana wa CHADEMA na watanzania wote ambao leo wanaiona
CHADEMA kama tumaini pekee la kuwakomboa, kauli hii tunaamini kama vijana
wa CHADEMA kuwa mamlaka za nidhamu hazitakaa kimya na kuiachia kauli ya
namna hii iachwe bila kutakiwa maelezo ya kina , tutaitisha kikao cha BARAZA
na tutaijadili kauli hii na kuwasilisha mapendekezo yetu kwenye vikao halali
vya chama .
4. Tunapenda kumwambia kuwa kama anaona kuwa yeye haendani na utamaduni
wa chama chetu na anakiona kuwa hakina uwezo wa kuongoza dola anafanya
nini kwenye chama ambacho anona kuwa hakiwezi kuongoza dola? Kwanini
atafute urais kwenye chama ambacho anaona hakiwezi kuongoza dola ?
anawatania watanzania? Ni heri akaenda kwenye hicho ambacho anaamini kuwa
kinaweza kuongoza dola , kwani lengo la chama chochote kile ni kuchukua dola
na sio vinginevyo.
5. Mwisho tunapenda kuwahakikishia vijana wote wa Tanzania na wananchi kwa
ujumla kuwa tayari CHADEMA kimejiandaa kikamilifu kuongoza dola na wasiwe
na hofu na maneno yaliyotamkwa na Mbunge huyu .
6. Natoa wito kwa Vijana wenzangu wote wa CHADEMA kuwa sasa tujiandae
kikamilifu katika kukabiliana na mtu yeyote yule ambaye ataonekana kuwa
kikwazo kwa chama chetu na wananchi kwa ujumla wake katika kuelekea
kuchukua dola 2015 .
Nawatakia kila la kheri katika ujenzi wa chama na tuendeleze operesheni ya ‘Vua
Gamba, Vaa Gwanda’ popote pale tulipo nchini.
Imetolewa leo Dar es Salaam, Mei 16, 2012 na;
John Heche
Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa.
No comments:
Post a Comment