Sunday, September 25, 2011

Maeneo Ya Wazi Kurudishwa Kwa Wananchi


NA  MAGRETH  KINABO – MAELEZO
 
   
WIZARA YA Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imejipanga kwa makini   ili kuhakikisha kuwa maeneo yote ya wazi yanarudishwa kwa wananchi ambapo matumizi yake yatakuwa kwa manufaa ya watanzania wote.
 
Aidha  wizara hiyo imesema kuwa itatoa muda maalum kwa watu wote walivamia maeneo  hayo kuondoka  wenyewe  na  utakapokwisha muda uliopangwa  itakuja kubomoa hivyo hakutakuwa na msamaha.(hakuna cha msalie mtume).
 
Kauli hiyo ilitolewa (leo)jana na Makamu Mwenyekiti  wa Kamati ya   Bunge  ya Ardhi na Maliasili na Mazingira, Abdulkarim  Shah, wakati akifunga maonesho ya  kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara ya wizara hiyo yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mashujaa, Mnazimmoja, jijini Dares Salaam.
 
Shah alitoa kauli hiyo ikiwa ni matazamio ya  miaka 50 ijayo ya wizara hiyo huku akisema maeneo hayo  yamepangwa kwa faida ya wananchi wote.
 
“Napenda kusisitiza kwamba  taaluma ya  upangaji miji inahitajika kutiliwa maanani na serikali haitakubali mipango hiyo kubadilishwa matumizi kiholela. Natoa rai hii kwa jamii kushirikiana na serikali kulinda maeneo ya wazi yaliyoko katika maeneo yao,” alisema Shah.
 
Aliwataka watendaji husika hasa wa halimashauri kutobalidilisha  matumizi ya ardhi .
 
Aliongeza kuwa wizara hiyo imeandaa mikakati ya kuwa na mipango shahidi ya uendelezaji miji itakayokidhi mahitaji ya idadi kubwa zaidi ya watu watakaoishi mijini.
 
Pia  kuwa na mipango itakayowezesha ujenzi wa miji nadhifu, ya kisasa na endelevu,kuzijengea uwezo halimashauri kusimamia na kudhibiti uendelezaji wa miji na kuwa na mipango ya matumizi ya ardhi kwa kila eneo la makazi nchini. 
 
“ Wizara imedhamiria kuongeza kasi ya upimaji wa ardhi nchini kwa matumizi mbalimbali pamoja na kupunguza gharama za upimaji, ambapo nchi itakuwa imejenga kituo cha kupokea na kusambaza picha za saltillite, vituo vingi zaidi cha upimaji vitajengwa,” alisema.
 
Makamu Mwenyekiti huyo  aliongeza kuwa wizara hiyo itaanza kutunza kumbukumbu za upimaji  na ramani kwa kutumia teknolojia ya kisasa, ambapo sasa inatumika  mikoa 15 baadae itakuwa mikoa yote  hadi wilayani kulingana na uwezo wa bajeti.
 
Alisema ili kuwawezesha wananchi kutumia ardhi kama mtaji  wizara itahakikisha kuwa mashamba ya wananchi vijijini kote nchini yanabainishwa yanapimwa na wamiliki wake wanapewa hatimiliki za kimila.
 
Alisema kwa upande wa Shirika la   Nyumba  la Taifa(NHC)  limejipanga kujenga nyumba 150,000 katika kipindi cha miaka 50 ijayo na kujenga nyumba kwa ubia kwa kuwashirikisha wawekezaji wengine.

No comments:

Post a Comment