Wajumbe wa Kamati Teule iliyoundwa na Bunge kuchunguza sakata la aliyekuwa
katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Ndg. David Jairo kuchangisha pesa kwa
ajili ya kupitisha Bajeti ya Wizara pamoja na hatua ya katibu Mkuu kiongozi
kuitolea taarifa ya uchunguzi mbele ya waandishi wa Habari kabla ya kuwasilishwa
Bungeni imeanza kukutana leo katika Ofisi ndogo ya Bunge chini ya uenyekiti wa
Mhe. Injinia Ramo Makani (CCM), mbunge wa Tunduru Kaskazini,
.
kamati hiyo inayoundwa na mhe. Goesbert Blandes (CCM), Mbunge wa Karagwe, mhe.
Mchungaji Israel Natse (Karatu-Chadema), mhe. Khalifa Suleiman Khalifa
(Gando-CUF) na mhe. Martha Jachi Umbulla (CCM). Mbunge wa Viti Maalum, inafanya
kazi kwa kuongozwa na hadidu tano za rejea ambazo ni:
kuchunguza utaratibu uliobainika wa kukusanya fedha kwa ajili ya kukamilishwa
kwa uwasilishaji wa Hotuba za bajeti za wizara bungeni na kwamba, hadidu hiyo ya
kwanza itakuwa na vipengele vitatu. Vipengele hivyo ni pamoja na: kuchunguza uhalali wa utaratibu huo kisheria na kwa mujibu wa kanuni, iwapo
fedha hizo huwa zinakasimiwa katika bajeti husika pamoja na matumizi halisi ya
fedha zilizokusanywa.
Hadidu rejea ya pili ni kupitia taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali kuhusu uchunguzi alioufanya kuhusiana na agizo la Katibu Mkuu wa Wizara
ya Nishati na Madini kuchangisha fedha taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo kwa
ajili ya kufanikisha uwasilishaji wa Bajeti ya Wizara hiyo Bungeni,
Hadidu rejea ya tatu ni kuchunguza mfumo wa Serikali kujibu hoja zinazotolewa
bungeni na taratibu za kuarifu Bunge matokeo ya utekelezaji wa hoja hizo".
Hadidu rejea hiyo ya nne ina vipengele viwili ambavyo ni kuchunguzwa kwa usahihi
wa utaratibu uliotumiwa na Katibu Mkuu Kiongozi kwa suala la Jairo na kubaini
iwapo utaratibu huo umeathiri dhana ya haki na madaraka ya Bunge.
Hadidu ya rejea ya tano ni kuangalia nafasi ya Mamlaka ya Uteuzi kwa ngazi za
Makatibu Wakuu katika kushughulikia masuala ya nidhamu ya anaowateua na ya
mwisho inawaelekeza wajumbe wa Kamati hiyo kuangalia mambo mengine yoyote yenye
uhusiano na uchunguzi huo.
Picha na Habari: Owen Mwandumbya wa Bunge
katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Ndg. David Jairo kuchangisha pesa kwa
ajili ya kupitisha Bajeti ya Wizara pamoja na hatua ya katibu Mkuu kiongozi
kuitolea taarifa ya uchunguzi mbele ya waandishi wa Habari kabla ya kuwasilishwa
Bungeni imeanza kukutana leo katika Ofisi ndogo ya Bunge chini ya uenyekiti wa
Mhe. Injinia Ramo Makani (CCM), mbunge wa Tunduru Kaskazini,
.
kamati hiyo inayoundwa na mhe. Goesbert Blandes (CCM), Mbunge wa Karagwe, mhe.
Mchungaji Israel Natse (Karatu-Chadema), mhe. Khalifa Suleiman Khalifa
(Gando-CUF) na mhe. Martha Jachi Umbulla (CCM). Mbunge wa Viti Maalum, inafanya
kazi kwa kuongozwa na hadidu tano za rejea ambazo ni:
kuchunguza utaratibu uliobainika wa kukusanya fedha kwa ajili ya kukamilishwa
kwa uwasilishaji wa Hotuba za bajeti za wizara bungeni na kwamba, hadidu hiyo ya
kwanza itakuwa na vipengele vitatu. Vipengele hivyo ni pamoja na: kuchunguza uhalali wa utaratibu huo kisheria na kwa mujibu wa kanuni, iwapo
fedha hizo huwa zinakasimiwa katika bajeti husika pamoja na matumizi halisi ya
fedha zilizokusanywa.
Hadidu rejea ya pili ni kupitia taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali kuhusu uchunguzi alioufanya kuhusiana na agizo la Katibu Mkuu wa Wizara
ya Nishati na Madini kuchangisha fedha taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo kwa
ajili ya kufanikisha uwasilishaji wa Bajeti ya Wizara hiyo Bungeni,
Hadidu rejea ya tatu ni kuchunguza mfumo wa Serikali kujibu hoja zinazotolewa
bungeni na taratibu za kuarifu Bunge matokeo ya utekelezaji wa hoja hizo".
Hadidu rejea hiyo ya nne ina vipengele viwili ambavyo ni kuchunguzwa kwa usahihi
wa utaratibu uliotumiwa na Katibu Mkuu Kiongozi kwa suala la Jairo na kubaini
iwapo utaratibu huo umeathiri dhana ya haki na madaraka ya Bunge.
Hadidu ya rejea ya tano ni kuangalia nafasi ya Mamlaka ya Uteuzi kwa ngazi za
Makatibu Wakuu katika kushughulikia masuala ya nidhamu ya anaowateua na ya
mwisho inawaelekeza wajumbe wa Kamati hiyo kuangalia mambo mengine yoyote yenye
uhusiano na uchunguzi huo.
Picha na Habari: Owen Mwandumbya wa Bunge
No comments:
Post a Comment