Thursday, June 7, 2012

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk Terezya Huvisa Akutana na Kamati ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Mazingira


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk Terezya Huvisa akizungumza na Kamati ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Mazingira kwenye ukumbi wa Hazina kulia Mwenyekiti wa Kamati hiuo James Lembeli kushoto Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Charles Kitwanga,Naibu katibu Mkuu Eng Ngosi Mwihava,Mh Zakhia Megji kikao hicho kimefanyika leo Mjini Dar es Salaam.Picha na Ali Meja

MILIONI 421.8 ZAPATIKANA KUCHANGIA MPANGO WA ELIMU KATA YA KIPAWA JIJINI DAR ES SALAAM

Mgeni rasmi wa harambee hiyo akimpa mkono wa asante mwakilishi wa kampuni ya Home Shopping Centre Bi Madiha Al Harthy (kushoto),Salma baada ya kuchangia sh. milioni 22...

Mbunge wa Jimbo la Segerea, Dk. Makongoro Mahanga (kulia), Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto) na Mwenyeji wa harambee ya kuchangia mpango wa elimu wa Kata ya Kipawa, Diwani wa Kata  hiyo Bonah Kaluwa, wakimuongoza Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa ambaye alikuwa mgeni rasmi kuingia ukumbini Katika hafla iliyofanyika jana usiku ndani ya hoteli ya Kilimanjaro (Kempiski hotel) jijini Dar es Salaam . 
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye harambee hiyo
Diwani wa Kata ya Kipawa Bonah Kaluwa, akitoa neno la shukurani kabla ya kuanza kwa harambee hiyo...
Mkurugenzi wa SONGAS Limited Bw;Christopher Ford(katikati),akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya dolla za kimarekani 10,000, mgeni rasmi wa harambee hiyo.kushoto meneja 
rasilimali Songas Bi Agatha Keenja...
 
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja (katikati) akipongezwa na Mgeni rasmi wa harambe hiyo baada ya kuchangia sh. 500,000...
 

eya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto), akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh.milioni 10, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, aliyekuwa mgeni rasmi katika harambee ya kuchangia mpango wa elimu Kata ya Kipawa, iliyofanyika Dar es Salaam juzi. Fedha hizo zilitolewa na Manispaa hiyo ambapo zaidi ya sh. milioni 400 zilipatikana.
Na Dotto Mwaibale

Wednesday, June 6, 2012

Dawa Za Kulevya Zaitikisa Iringa



Na Mwandishi Wetu

BIASHARA ya dawa za kulevya imeshika kasi mkoani Iringa huku vigogo kadhaa wakitajwa kuhusika, Kwanza Jamii-Iringa linaripoti.
Taarifa zinaeleza kwamba, wafanyabiashara kadhaa maarufu mkoani humo wanatajwa kujihusisha katika usambazaji na utumiaji wa dawa hizo, hususan cocaine, heroin na Mandrax.
Kundi rika la vijana wenye umri kati ya miaka 18 na 35 ndilo linaloongoza kwa biashara hiyo kwa utumiaji na usambazaji, huku bhangi ikiwa inaongoza miongoni mwa orodha ya dawa za kulevya.
“Huwezi kuipiga vita biashara ya dawa za kulevya ikiwa vigogo wenyewe ndio wanaosambaza na kutumia. Wapo wanajulikana, lakini hatujui ni kwa vipi serikali inashindwa kuwakamata,” kimeeleza chanzo chetu cha habari.
Inaelezwa kuwa, wafanyabiashara kadhaa wa mjini humo, ambao baadhi wanadaiwa kuwemo kwenye orodha ya vigogo 58 wa dawa za kulevya iliyopelekwa kwa Rais Jakaya Kikwete mwaka 2006, ndio miungu-watu wanaojificha kwenye mwavuli wa biashara zao halali pamoja na kusaidia jamii.
Taarifa zinaeleza kwamba, vigogo wengi na hasa wenye fedha, ndio watumiaji wakubwa wa dawa za viwandani kama heroin na cocaine kwa vile hawawezi kwenda kununua bhangi mitaani kutokana na hadhi zao, huku kundi kubwa la vijana likitajwa kutumia zaidi bhangi.
Wananchi kadhaa waliohojiwa na gazeti hili kwa masharti ya kutotajwa majina yao, walisema matumizi ya dawa za kulevya mkoani humo yanazidi kushika kasi licha ya serikali kusema yamepungua.
“Huku mitaani sisi ndio tunaowaona watumiaji, wanaongezeka kila wakati na hakuna juhudi za kuwapunguza, hasa vijana ambao wanazidi kuathirika na matumizi hayo,” walisema wananchi hao.
Kauli hiyo ya kukithiri kwa matumizi ya dawa za kulevya iliungwa mkono na Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kitanzini iliyo katikati ya Manispaa ya Iringa, Raphael Magata, ambaye alisema matumizi ya dawa za kulevya kwa vijana yanazidi kuongezeka.
Magata alisema kwamba, pamoja na juhudi kubwa zinazofanywa na serikali pamoja na asasi mbalimbali za kijamii kuelimisha juu ya madhara yake, lakini idadi ya vijana wanaojihusisha na biashara hiyo inazidi kuongezeka, hivyo kuitaka jamii ishiriki kupambana ili kuokoa nguvu kazi isipotee.
“Vijana wengi hivi sasa wanajihusisha na utumiaji wa dawa za kulevya ingawa serikali inajitahidi kuwalimisha madhara yake kwa kushirikiana na asasi binafsi. Madhara yake ni makubwa kwa sababu yanachangia pia maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi,” alisema Magata.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Peter Kakamba, alisema kwamba, jeshi lake linajitahidi kupambana na matumizi na biashara ya dawa hizo za kulevya, kwa kushirikiana na jamii kupitia Ulinzi Shirikishi.
Soma zaidi ...http://www.kwanzajamii.com

Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki wala Kiapo

Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) leo wameapishwa rasmi kushika madaraka hayo huku Tanzania ikiwa na Wawakilishi tisa katika Bunge hulo.

Wabunge hao waliapa baada ya kupatikana Spika wa mpya wa Bunge hilo ambapo safari hii ikiwa ni Uganda kushika Uongozi huo wa Juu wa Bunge na Mwana Uchumi, Margareth Zziwa kuchukua nafasi hiyo.

Wabunge wote wa Tanzania katika Bunge la Jumuiya ya Mashariki waliokula kiapo hii leo ni pamoja na Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania kwenye Bunge EALA, Alhaj Adam Omar Kimbisa na Katibu wake, Mh Shy-Rose SaddrudinBhanji.

Wengine ni Mhe. Anjela Charless Kizigha, Mh. Maryam Ussi Yahya,Mh.Nderkindo Perpetua Kessy, Dkt Twaha Issa Taslima, Mhe. Abdullah Ali Hassan Mwinyi, Mhe Bernard Musomi Murunyana Mhe. Charles Makongoro Nyerere na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta anaeingia kwa wadhifa wake wa Uwaziri.

Wabunge hao wameapisha pamoja na wabunge wenzao wa Kenya, Uganda, Rwanda na katika picha juu ni Waziri wa Afrika Mashariki na mbunge wa Urambo Mh Samwel Sitta akiapa katika bunge hilo jana jijini ArushaSOURCE: FATHER KIDEVU BLOG

MBUNGE WA SEGEREA AWATAKA WADAU WA ELIMU KUJITOKEZA KATIKA HARAMBEE YA KATA YA KIPAWA KATIKA HOTELI YA HYATT KILIMANJARO

Diwani wa Kata ya Kipawa Manispaa ya Ilala Dar es Salaam, Bonah Kaluwa (kushoto), akiwa katika moja ya mikutano ya maendeleo kwenye kata yake. Kulia ni Katibu  wa Kata hiyo Amina Sabo na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Karakata, Greyson Malick. (PICHA NA DOTTO MWAIBALE)
 
 
Na Dotto Mwaibale

MBUNGE wa Jimbo la Segerea Dk. Makongoro Mahanga amewataka wadau wa elimu kujitokeza leo kuchangia mfuko wa elimu wa Kata ya Kipawa katika harambee itayoongozwa na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa katika Hoteli ya Kilimanjaro Kempiski.

Alisema Kata ya Kipawa ni moja ya kata iliyopo katika jimbo la Segerea na Manispaa ya Ilala zenye upungufu mkubwa wa miundombinu na vifaa katika shule zake za msingi na za sekondari za serikali.

Alisema upungufu huo ni pamoja na uchache wa shule, upungufu wa madarasa, madawati, matundu ya vyoo, ofisi za walimu, meza na viti vya walimu, maabara na nyumba za walimu.
" Upungufu huu wa mahitaji katika shule za kata ya Kipawa, ni tatizo la mkoa mzima wa Dar es Salaam, na wilaya nzima ya Ilala hivyo ni wajibu wetu kusaidia". alisema Mahanga

Alisema katika suala la elimu serikali ya awamu ya nne imefanya mengi mazuri ingawa bado kuna changamoto kadhaa ambapo kwa mkoa wa Dar es Salaam,  kumekuwepo na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaosoma shule za awali, shule za msingi na shule za sekondari.

Aliongeza kuwa kwa sasa kuna wanafunzi 26,121 wa shule za awali katika mkoa wa Dar es Salaam, kati yao wanafunzi 7,499 wako katika wilaya ya Ilala. Mkoa wa Dar es Salaam pia kwa sasa una wanafunzi 510,269 wanaosoma shule za msingi, kati yao wanafunzi 152,135 ni wa wilaya ya Ilala.

Alisema  kuna wanafunzi 204,684 wa shule za sekondari katika mkoa wa Dar es Salaam, kati yao wanafunzi 57,890 wako katika wilaya ya Ilala. Katika mkoa wa Dar es Salaam, kuna shule 315 za sekondari, kati yake shule 135 ni za serikali.

" Nguvu za wananchi zimetumika sana hasa katika ujenzi wa shule za sekondari nchini na kuungwa na serikali ambapo kwa mkoa   wa Dar es Salaam kati ya shule hizo za serikali 135, shule 124 ni za wananchi zilizojengwa kwa nguvu za wananchi wakishirikiana na Halmashauri za wilaya." alisema Mahanga.

Alisema shule hizo 124 za wananchi za mkoa wa Dar es Salaam, wilaya ya Ilala ina shule 40 za sekondari za wananchi, ambazo karibu zote zimejengwa kuanzia mwaka 2006.

Alisema Shule hizo nyingi zinachangamoto na upungufu wa vyumba vya madarasa 5,526, kati yake wilaya ya Ilala ina upungufu wa madarasa 1,459, ofisi za walimu 466,nyumba za walimu 14,788.

Alisema katika mkoa wa Dar es Salaam kuna upungufu wa madawati 58,764 kwa shule za msingi na 45,349 kwa shule za sekondari. Kati ya hizo wilaya  ya Ilala ina upungufu wa madawati 18,030 kwa shule za msingi na madawati 19,534 kwa shule za sekondari.
Alisema matundu ya vyoo 18,558 yanahitajika kwa mkoa wa Dar es Salaam, huku wilaya yenu hii ya Ilala ikihitaji matundu ya vyoo 4,886.

Alisema katika uchangia wa elimu hatuwezi kuiachia serikali pekee, kwani uwezo wa serikali yetu ni ndogo hivyo alitumia fursa hiyo kuwapongeza viongozi wa kata ya Kipawa wakiongozwa na diwani wao, Bonnah Kaluwa kwa kubuni mradi wa uchangiaji miundombinu ya shule katika kata hiyo.

Tuesday, June 5, 2012

BATA ZA DOGO RAMA WA TWANGA PEPETA...

 

Nyota wa Muziki wa Dansi Dogo Rama(kushoto) aki- shoo luv kiaina na mshikaji wake ndani ya viwanja vya Leaders Club , Kinondoni jijini dar es salaam Jumapili wiki iliyopita.

CCM Wametua Njombe Leo..

 








Picha zote: Bashir Nkoromo